Friday, November 11, 2011

Breaking News; Mlimani Kumechafuka, ni mabomu na risasi zinarindima

Mwandishi wetu kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam anaripoti kuzuka kwa vurugu hivi punde katika viunga vya chuo kikuu Dar es salaam. Kiini cha vurugu hizo kinaelezwa kuwa ni ubabe wa serikali kwa kujibu hoja kwa kutumia risasi na mabomu, taarifa zaidi kutoka kwa baadhi ya wanafunzi zinaeleza kuwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wengine wanaitaka serikali kuwapatia haki yao "mikopo" pamoja na fedha za kujikimu lakini cha ajabu si waziri wa elimu Dk Shukuru Kawambwa wala rais Jakaya Kikwete aliyefungua mdomo wake kujibu hoja badala yake wasomi hao wanatishiwa kufungwa midomo kwa nguvu ya risasi na mabomu ambayo yanaendelea kurindima chuoni hapo.
BLOG HII INALAANI VIKALI UBABE HUU NA KUWAPA POLE WANAFUNZI WOTE WANAAONEWA BILA SABABU ZA MSINGI.

No comments:

Post a Comment