Sunday, November 27, 2011

University of Dar es salaam Business School -UDSM


                  (Baadhi ya classmates wa UDBS mwaka wa pili waki-pay attention kwa lecture)


University of Dar es salaam Business school (UDBS) is a school of business that seeks to become a world class business school that is responsive to national, regional and global socio-economic developmental needs through innovation, knowledge creation and application.Kwa mpango huo mzima sie kama students of this school let us cooperate and make things happen.Japo kwa kipindi hiki tunapoanza juma la nane mambo ni mengi zaidi....Always lets pray for our Lord God atuwezeshe kufika pale tunapo-wish kufika.

Friday, November 11, 2011

Breaking News; Mlimani Kumechafuka, ni mabomu na risasi zinarindima

Mwandishi wetu kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam anaripoti kuzuka kwa vurugu hivi punde katika viunga vya chuo kikuu Dar es salaam. Kiini cha vurugu hizo kinaelezwa kuwa ni ubabe wa serikali kwa kujibu hoja kwa kutumia risasi na mabomu, taarifa zaidi kutoka kwa baadhi ya wanafunzi zinaeleza kuwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wengine wanaitaka serikali kuwapatia haki yao "mikopo" pamoja na fedha za kujikimu lakini cha ajabu si waziri wa elimu Dk Shukuru Kawambwa wala rais Jakaya Kikwete aliyefungua mdomo wake kujibu hoja badala yake wasomi hao wanatishiwa kufungwa midomo kwa nguvu ya risasi na mabomu ambayo yanaendelea kurindima chuoni hapo.
BLOG HII INALAANI VIKALI UBABE HUU NA KUWAPA POLE WANAFUNZI WOTE WANAAONEWA BILA SABABU ZA MSINGI.

A New Collection of Nyerere's Work to be Published Next Week !

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg5qRwZPXRiYMudz02ATSBKfQ1XOML1zukksFYrUTK_MG__fqVCZbLWzWZo4IZFcBWpFL4HohEWj9iWmqPXhRrQwkKKq2lTFvWunxQsNQvsNYXoagHNjP4UEWkHWNhinlLB0ZvGdHhJHh8/s400/90638100929850L.gif
Report from Detroit, USA
Twelve years after his death Mwalimu Julius Kambarage Nyerere will be immortalized once again after a new collection of his speeches and other literal works will be published by the foundation bearing his name. On November 16th, 2011 the Mwalimu Nyerere Foundation will release three collections of Nyerere’s works at a gala which will be followed by a public symposium.

The new collection of Nyerere’s works cover the years between 1974 and 1999. The three books will be available at the foundation and at the Oxford Printing Press in Dar-es-Salaam. Other arrangements are being made to have the books available at various bookstores and libraries around the country.

This new collection contains over 120 speeches that the Founding Father Mwalimu Nyerere gave on various national and international issues which were very dear to his heart as a political philosopher, Africa’s senior Statesman, and a humanist of a distinguished caliber. There are three volumes of the new collection which are titled Freedom and Liberation (Uhuru na Ukombozi wa Africa), Freedom, Non-Alignment and South-South Cooperation (Uhuru, Kutofungamana na Ushirikiano wa Nchi za Kusini), and Freedom and A New World Economic Order (Uhuru na Mfumo Mpya wa Uchumi Duniani).

Sunday, November 6, 2011

Haijapata kutokea---- Thomas Nyimbo avunja ngome ya CCM Njombe Aweka Rekodi!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgORk-dmfO6NnGdrt6dcJbHBl7ZVFVXkvoYosTQnhBJf70GgRsN40yb-NV8AoNFX6lDi-Eyw6tvn-VFBI9XrnpC9UMEtlQ54EJw0b1BVQHMbb-eaG7zVWLpp-kKBXKDdBxmXKeLaFMdg-Y1/s1600/NYIMBO.JPG
PICT0406.JPG‎Picha ya ofisi mpya ya CHADEMA jimbo la Njombe Magharibi
Wote tunajua mambo ya ajabu yaliyofanywa na CCM wakati wa uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010 katika Jimbo la Njombe Magharibi. Baada ya kufanyiwa hujuma ndani ya CCM na baadae akigombea kwa Chadema Thomas Nyimbo aliamua kutokwenda mahakamani na badala yake aliamua kukata rufaa kwa wananchi.
Kwa ufupi CCM Njombe Magharibi iko taabani na ushahidi ni ofisi hii ambayo Mh.Nyimbo nbaada ya kufanikiwa kupata wanachama katika Wilaya nzima ya Njombe (Wanging'ombe) sasa amejenga ofisi hii ambayo sijapata kuiona katika Mikoa mingi iliyopiga hatua kimageuzi. Hii ni ofis ya Wilaya mpya ya Wanging'ombe .
Baadhi ya Majibu ya Wadau haya hapa
Yeye alisema yupo tayari kuwa Mlezi wa Chama wa Mkoa mpya wa Njombe so na hataki mkuwa kwenye ngazi yoyote ya maamuzi ila kushikiri kujenga Chama. Mpaka sasa amenunua pikpiki 8 kwa ajili ya uenezi katika Wilaya mpya ya Wanging'ombe na ameshagharimia safari za waenezi walioenda hadi Ludewa na Makete. Huyu Mzee ni mfano wa kuigwa sana

Kwa kweli huyu mzee ni mfano wa kuigwa maana anakijenga chama na hapo hapo analeta maendeleo kwa wananchi tena akiwa nje ya bunge sipati picha kama angekuwa mbunge wananchi wa jimbo hilo wangepata maendeleo makubwa! Miaka 4 siyo mingi kama Mungu akimpa uhai na nguvu.

Nilipita huko Njombe september Mzee Nyimbo amekuwa akifungua matawi kijiji kwa kijiji na kuvunjavunja ngome ya CCM mpaka sasa bendera za CHADEMA zinapepea kila kijiji na ndani ya vitongoji, kikubwa ni wadau kumpa support katika uchaguzi wa serikali za mitaa ili tusimike wenyeviti wa vitongoji na vijiji wa kutosha ili kusafisha njia ya 2015. Lengo ni kusajili T2015CDM.

Mafisadi CCM lazima wavue gamba;Willison Mukama

http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2011/04/Wilson-Mukama-2.jpg
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama, amesema yeye ni sawa na mtu aliyeteuliwa kufanya kazi ya kunyonga mkosaji aliyehukumiwa adhabu hiyo na Mahakama, hivyo hawezi kuogopa kutekeleza hukumu hiyo.

Akifafanua kauli hiyo jana mjini Morogro, Mukama alisema uamuzi wa ngazi za juu wa CCM ukishatolewa kuhusu kuvua gamba watuhumiwa wa ufisadi, hakuna kiongozi atakayepuuza kuutekeleza.

“Ufisadi unasemwa dhahiri na wananchi kwa kuwataja watuhumiwa hadharani wakiwahusisha ana EPA (Akaunti ya Malipo ya Nje ya Benki Kuu), Dowans, ununuzi wa rada na Richmond … na vikao vya chama vimetoa uamuzi.

“Kilichobaki ni utekelezaji tu…na hukumu ikishatolewa na Mahakama hakuna njia nyingine isipokuwa kutekeleza agizo hilo,” alisema Katibu Mkuu huyo alipokuwa akizungumzia madai, kwamba anaogopa kutoa barua za kujivua gamba kwa watuhumiwa wa ufisadi.

Akihutubia mahafali ya wanafunzi wanachama wa CCM wanaomaliza Chuo Kikuu cha Mzumbe Morogoro, Mukama alisema hataogopa kusimamia kikamilifu uamuzi wa chama hicho wa kuwatosa watuhumiwa hao.

Alisema vitendo vyao vimesababisha CCM na Serikali ichafuke mbele ya Watanzania.

Mbali na kuwavua gamba, Mukama alisema CCM pia itashughulikia suala la wafanyabiashara wasio waadilifu wanaojipenyeza ndani ya chama hicho, na itapambana na saratani ya kujilimbikizia madaraka na kukiondoa chama hicho katika utegemezi wa matajiri na wahisani wanaokiweka pabaya.

Alisema, hakuna mwananchi asiyejua kuwa ndani ya CCM wapo viongozi wenye nyadhifa kubwa wanaotuhumiwa kwa ufisadi kuanzia wa EPA, Richmond, Dowans, Rada na kashfa nyingine.

Katibu Mkuu huyo alisisitiza kwamba ili kukisafisha chama hicho mbele ya jamii na kukifanya kikubalike katika uchaguzi wowote, ni lazima watuhumiwa hao watoswe ili kurudisha imani kwa Watanzania.

Mukama alionesha katuni aliyodai imemchora hivi karibuni, akiwa na barua mkononi ikionesha kuwa ameshindwa kutoa uamuzi na kusisitiza kuwa uamuzi huo ni wa chama, hivyo utatekelezwa kama ilivyopangwa.

Awali katika risala ya wanafunzi hao, walitaka viongozi wote wa CCM kujikita kuwaletea maendeleo wananchi, ili baadaye wapimwe kwa kazi zao.

Wanachama hao waliwataka viongozi wahubiri amani badala ya kuendeleza malumbano na vyama vya upinzani na kuwataka watumishi wa Serikali kuachana na siasa wakati wakiwa watumishi wa umma.
Website Rasmi ya Chama Cha Mapinduzi - CCM

Ansbert Ngurumo: Muone, kichwa kama CCM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjs8wny5CiVKPSiBZBLde2ff4-7J8B3crcl7ur2AZxjnUNYPwe98GqaQxCR2XiaGBBJYsOl_rigN8RqJJVetWZnB3n5uyqbb6lkKBBQaIOXXfJjQBZwLA5SUPyOHVMuygeNIJJFhbBJeoTr/s220/Ansi+13.11.2007.bmp
NAWAHUSUDU, na wakati mwingine nawashangaa sana Watanzania wenzangu wanaojipanga kuomba uongozi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Hawa ni watu waliojilipua. Wanahitaji nguvu ya ziada.
Maana zama zimebadilika. CCM sasa kimekuwa mzigo mzito usiobebeka kwa kila Mtanzania.
Hata viongozi wa chama, akiwamo Rais Jakaya Kikwete, wameanza kutambua kwamba kuongoza CCM si jambo la kujivunia tena. Ni changamoto kubwa sana. Ni adhabu!
Wanachama nao wamefika mahali wanaona aibu kujitambulisha kama wana CCM, kwa sababu wanaogopa kuzomewa. Siku hizi, ukitaka kulinda heshima yako, fiche u-CCM wako.
Baadhi ya makada maarufu, wakiwamo wabunge, wamekiri kwangu kwamba katika maeneo mengi ya nchi hii, chama hakiuziki, hakibebeki. Wanasisitiza kwamba tofauti na zamani ambapo chama kilikuwa nyenzo muhimu inayotumika kuwabeba wanasiasa wanaogombea uongozi, sasa hivi imefika mahali ambapo wagombea ndio wanatarajiwa kukibeba chama.
Maana yake ni kwamba ukitaka kugombea uongozi CCM lazima uwe na pesa nyingi za kuhonga wananchi na kununua ushindi, na uwe na uhakika wa kuitumia dola dhidi ya wapinzani wako.
Ni siri iliyo wazi kwamba wabunge wengi wa CCM waliochaguliwa mwaka jana, walipita kwa sababu ya majina yao, na jitihada binafsi; si kwa sifa ya chama.
Baadhi ya wale niliozungumza nao, wamekiri kwamba katika majimbo yao, wao ndio CCM – maana ndio wanaokibeba chama badala ya chama kuwabeba wao. Mmoja wao aliniambia kwamba ingawa yeye ni mbunge wa CCM, ana uhakika kwamba pale jimboni kwake hakuna CCM, bali kuna CHADEMA.
Maana yake ni kwamba wabunge hao wangechaguliwa tu, hata kama wangegombea kupitia chama kingine.
Tafsiri ya haraka ni kwamba iwapo wabunge hao wa CCM wakihama chama leo, wataondoka na wapiga kura wao.
Na hii ndiyo tofauti kubwa ya sasa kati ya CCM na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mbele ya umma.
Kwa asilimia kubwa, chuki ya wananchi dhidi ya CCM imegeuka ushabiki na mapenzi kwa CHADEMA. Pale ambapo kada au mgombea wa CCM anaona aibu kujinadi kwa chama chake, yule wa CHADEMA anajua kuwa asipotumia mwamvuli wa chama kujinadi anakuwa na nafasi ndogo ya kushinda.
Ile jeuri ya wanachama na mashabiki wa CCM kutembea kifua mbele wakiwa wamevaa mashati na fulana na kijani na njano mitaani, imenyauka.
Ndiyo maana kada mmoja wa CCM aliyekuwa mstari wa mbele katika uchaguzi mdogo wa Igunga aliniambia kuwa ilifika mahali wakagundua kwamba kijani chao ni nuksi, kinachukiwa na kitawanyima fursa ya kufanya kampeni kwa amani.
Akasema, “Tuligundua hilo, tukawa hatuvai mashati na fulana za kijani, bali tunavaa kiraia, ndipo tunapata uhuru wa kupita mitaani na kuomba kura nyumba kwa nyumba.”
Hii ndiyo sababu inayowafanya CCM kuandaa mikutano ya hadhara kwa gharama kubwa mno, ikuhusisha kubeba wananchi kwenye malori na mabasi kutoka sehemu za mbali na kuwaleta mahali pa mkutano, tena baada ya kuwaahidi au kuwagawia pesa au fadhila nyinginezo.
Ndiyo maana vijana waendesha pikipiki na daladala hawaendi kwenye mikutano ya CCM kwa hiari. Lazima wahongwe mafuta na kupewa pesa ya kula; wakati vijana hao hao hushindana wao kwa wao kununua mafuta na kujaza matanki ya pikipiki au magari yao kwenda kwenye maandamano na mikutano ya CHADEMA.
Hiii ni sehemu ya maelezo kwa nini CCM hawawezi kushinda bila kutegemea nguvu ya pesa na polisi. Wakati tuliomo ni ule wa chama tawala kuishi kwa kudra za dola, huku upinzani ukikua kwa kasi ya ajabu kwa kudra za nguvu ya umma.
Miaka kadhaa iliyopita, katika maeneo mengi ya nchi hii, ilikuwa aibu na kejeli mtu kujinadi kuwa mpinzani. Sasa hivi ni jambo lisilo la kujivunia mtu kujitambulisha hadharani kuwa ni mwana CCM.
Miaka saba iliyopita, wananchi kadhaa huko vijijini waliwahi kuniambia kuwa mtu anayetamani kugombea uongozi, kama ana nia ya kushinda apitie CCM.
Mwaka huu, wananchi wale wale wamenieleza kwamba kama mtu anataka kushindwa agombee kwa tiketi ya CCM.
Kama ambavyo baadhi yetu tumesema huko nyuma, CCM kinakufa. Hata hiyo idadi ya wanachama wanayotangaza, milioni nne, haipo. Ni propaganda tu za kisiasa.
Ikumbukwe kuwa waasisi wa CCM wanazidi kufa. Wengine wanazeeka. Wengine wamekihama chama. Sehemu kubwa ya idadi ya Watanzania ni vijana. Ni wao wamezaliwa miaka ya harakati za mageuzi ya kisiasa. Wengi wao wamejiunga kwenye vyama vya mageuzi. Sasa hivi hata watoto wadogo wanasalimiana kwa kunyosha vidole viwili, ishara ya ushindi inayotumiwa CHADEMA.
Shule za sekondari na vyuo vya elimu ya kati na ya juu vimejaa wanafunzi wasiokipenda CCM. Katika mazingira haya, CCM kinazidi kukosa mvuto, na wanachama wa CCM wanazidi kupungua.
Kinawapata wapi hao milioni nne? Kama kina wanachama wengi hivyo, mbona hawakubali kuhudhuria mikutano ya CCM bila kubembelezwa na kuhongwa?
Kama CCM kingekuwa na idadi kubwa kiasi hicho, CHADEMA kingepata wapi jeuri ya nguvu ya umma?
Chuki ya wazi dhidi ya CCM inasababishwa na maisha magumu waliyonayo wananchi. Udhaifu wa serikali ndio umekiua CCM, maana kimegeuka chama cha viongozi waongo, wasioaminika.
Mwaka huu, wakati tunatimiza miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika, tunatimiza pia miaka sita ya utawala wa Rais Kikwete.
Ni miaka sita ya shida na umaskini unaosababisha chuki ya wananchi dhidi ya Rais Kikwete. Hatujasahau kwamba mwaka 2005 Kikwete aliomba kura akiahidi maisha bora kwa kila Mtanzania. Yako wapi?
Utafiti uliofanywa na taasisi ya takwimu, ya serikali hii hii, kuhusu mapato binafsi ya kaya, unaonyesha kuwa mwaka huo (2005) Watanzania waliokuwa wanakula mara moja tu kwa siku walikuwa asilimia 34 ya wananchi wote.
Mwaka huu, idadi ya Watanzania wanaobahatisha mlo mmoja tu kwa siku imeongezeka hadi asilimia 41. Maana yake, idadi ya Watanzania wanaoshinda au kulala njaa katika miaka mitano ya Rais Kikwete imeongezeka kwa asilimia saba!
Hawa wana sababu ya kuiamini CCM? Wana sababu ya kuipenda CCM? Wana sababu ya kuiamini serikali ya Rais Kikwete? Wameyaona maisha bora waliyoahidiwa na JK?
Utafiti huo huo unaonyesha kuwa asilimia 42 ya watoto wote wenye miaka mitano katika kipindi hichi hicho wamedumaa. Kama wazazi wao wanakula mara moja tu kwa siku, tena kwa kubahatisha, watoto wao watawezaje kukua vizuri na kupata maisha bora? Wazazi wa watoto hawa waliodumaa wana sababu za kushangilia miaka 50 ya utawala wa CCM na sita ya maisha magumu ya JK?
Taifa la watoto waliodumaa linajivunia miaka 50 ya CCM na sita ya Kikwete? Taifa la namna hii linaona manufaa ya kuongozwa na CCM yenye magamba au isiyo na magamba?
Takwimu hizo hizo za serikali zinaonyesha kuwa katika kipindi kile kile walichoahidiwa maisha bora, asilimia 54 ya Watanzania wote hawali nyama kabisa!
Tutawezaje kujivunia afya na usitawi wa watu wetu kama wanakosa hata virutubisho muhimu kama protini itokanayo na nyama?
Hii ina maana gani kwa taifa linalosemekana kuwa la tatu kwa wingi wa mifugo katika Afrika, ambalo zaidi ya nusu ya watu wake hawali nyama?
Mambo haya na mengine ndiyo yamewafanya baadhi ya watu kuogopa kujitambulisha kuwa wana CCM.
Na sasa nimesikia katika baadhi ya maeneo nchini, CCM imegeuka tusi miongoni mwa vijana. Ukimuudhi mtu siku hizi, akakosa tusi la kistaarabu dhidi yako, atakwambia: “Muone, macho kama CCM!”

UDSM;Assessment by Panel of Experts

http://www.udsm.ac.tz/images/news_story.jpg
As one of the activities that marks the 50 years anniversary of the University of Dar es Salaam an International panel of experts has been appointed to assess it, its programmes and delivery processes against its official mission and goals, and to recommend ways in which University of Dar es Salaam ought to realign itself so as to ensure optimal performance in the changing circumstances of the 21st century. Read more http://www.udsm.ac.tz/